
Spread the love
ℹ️ We have been made aware of a video believed to show a footballer using a mobile phone whilst driving. This has been passed to the relevant department. Thanks for letting us know 👍
— MerPolCC (@MerPolCC) August 13, 2018
MSHAMBULIAJI wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohammed Salah ameingia matatizoni na polisi wa Merseyside baada ya kuibuka kwa video mitandaoni akionekana kuendesha gari huku akiwa anatumia simu yake ya mkononi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Polisi jijini Liverpool wamethibitisha tukio hilo kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa twitter na kusema kwamba video hiyo imekabidhiwa kwenye kitengo husika.
ℹ️ We have been made aware of a video believed to show a footballer using a mobile phone whilst driving. This has been passed to the relevant department. Thanks for letting us know 👍
— MerPolCC (@MerPolCC) August 13, 2018
Video hiyo ambayo ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mchezaji huyo akiwa anatumia simu yake huku akiwa amesimamisha gari lake kwa muda baada ya kuzingirwa na mashabiki wakiwemo watoto, kisha akaamua kuondoa gari akiwa bado anatumia simu yake.
Hata hivyo uongozi wa klabu ya Liverpool ulitoa taarifa ya kuwa imewafahamisha polisi wa Merseyside kuhusu video hiyo baada ya kushauriana na mchezaji mwenyewe na kujua nini kilitokea wakati tukio hilo linafanyika.
More Stories
Simba yalazimisha sare Sudan, yaongeza pointi CAF
Manula ‘out’ dhidi ya Al Merreikh
Mtifuano VPL