Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Dereva wa mbunge auwawa na polisi
KimataifaTangulizi

Dereva wa mbunge auwawa na polisi

Spread the love

DEREVA wa Mbunge wa Jimbo la Kyaddondo Mashariki  nchini Uganda,  Robert Kyagulanyi  Bobi Wine, Yasin Kawuma amefariki baada ya kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa na polisi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bobi Wine amedai kuwa dereva wake ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi akiwa ndani ya gari la mbunge huyo, wakidhani kuwa aliyekuwa kwenye gari ni yeye.

Mbunge huyo ambaye pia ni msanii wa muziki nchini humo, ameandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa walikuwa eneo linalojulikana kama Arua kwenye kampeni wakati mauaji hayo yalitokea.

Bobi Wine na viongozi kadhaa wa upinzani walikuwa eneo hilo kumuunga mkono mgombea huru Kassiano Wadri anayeshiriki katika uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi ya Mbunge wa jimbo hilo, Ibrahim Abiriga aliyeuawa.

Wakati wa kampeni hizo zikiendelea kulizuka vurugu kati ya wafuasi wa Wadri na wale wa mpinzani wake katika uchaguzi huo wa chama cha NRM, Tiperu Nusura.

Msemaji wa polisi Emilian Kayima, anasema watu waliokuwa wamevaa shati za kampeni za mgombea Wadri, walianza kuurushia mawe msafara wa rais hali ambayo ilisababisha polisi kufyatua risasi.

“Mwendo wa saa kumi na mbili jioni msafara wa rais ulishambuliwa na wahuni katika manispaa ya Arua wakati rais alikuwa anaondoka uwanja wa Boma ambapo alikuwa amefanya mkutano wa mwisho,” amesema Kayima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!