Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi
Habari za Siasa

Mbunge wa Chadema awamwaga Polisi

Pascal Haonga, Mbunge wa Mbozi (mwenye kombati nyeusi) akiwa na wadau wengine wakishangilia
Spread the love

MBUNGE wa jimbo la Mbozi mkoani Songwe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pascal Haonga na wenzake wameshinda kesi iliyokuwa inawakabili katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha makosa dhidi ya watuhumiwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Haonga na wengine Katibu wake Wilfred Mwalusamba na Mashaka Mwampashi walikuwa wakikabiliwa na makosa ya kuvuruga mkutano wa uchaguzi wa baraza la mji mdogo wa Mlowo kosa la pili na la tatu kuwazuia askari kutekeleza majukumu yao makosa hayo wanadaiwa kuyatenda tarehe 28 Agosti, mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Nemes Chami alisema katika mashtaka yote matatu yalikuwa yanawakabili, hakuna hata sehemu moja upande wa mashtaka uliothibitisha.

“Hakuna mahali walipoonesha kwamba washtakiwa hawa waliwazuia askari kutekeleza majukumu yao na hakuna mahali walipo thibitisha kwamba washtakiwa walilazimisha kurudi ukumbini baada ya kutolewa nje” Alisema Chami.

Baada ya kusoma hukumu hiyo hakimu huyo alisema kuwa kama kuna upande ambao haujarizika na hukumu hiyo una haki ya kukata rufaa ndani ya muda.

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!