Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema, NCCR-Mageuzi wapigwa ‘stop’ Tarime
Habari za SiasaTangulizi

Chadema, NCCR-Mageuzi wapigwa ‘stop’ Tarime

Spread the love

MSIMAMIZI Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata ya Turwa wilayani Tarime, Mara amesitisha mikutano yote ya kampeni ya vyama vya upinzani kwenye kata hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hizo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kupitia barua inayodaiwa kutolewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Turwa, Peter Julius yenye kichwa cha habari; KUSITISHWA KWA KAMPENI ZA UCHAGUZI KWA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI KUANZIA TAREHE 10/08/2018 HADI 11/08/2018’.

Sehemu ya barua hiyo inaeleza kuwa, hatua hiyo imekuja baada ya NCCR-Mageuzi kudaiwa kukiuka sheria ya taifa ya uchaguzi.

“Nakujulisha kwa kufuatia chama tajwa hapo juu kukiuka kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343, Maadili ya Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka 2015, Kamati ya Maadili ya Uchaguzi Kata ya Turwa kupitia kikao kilichoketi tarehe 10/08/2018 kimesitisha kampeni za chama hicho kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 10/08/2018 hadi 11/08/2018,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.

Kabla ya NCCR-Mageuzi kusitishwa kufanya kampeni kata ya Turwa, Chadema pia ilisitishwa kufanya kampeni za udiwani kwenye kata hiyo.

Barua hiyo imeeleza kwamba, kuanzia leo kampeni zitaendelea kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) pekee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!