Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge mwingine Chadema ang’oka
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge mwingine Chadema ang’oka

Spread the love

JINAMIZI la kukimbiwa na wabunge na madiwani linazidi kuitafuna Chadema, ambapo jana tarehe 30, 2018 Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga kupitia chama hicho ametangaza kujivua uanachama na kuhamia chama tawala CCM, Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi huo wa Kalanga unakuja ikiwa zimepita siku mbili tangu aliyekuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara kutangaza kujivua ubunge, uanachama na nyadhifa zote alizokuwa nazo Chadema na kurudi CCM kwa kile alichodai kuwa Chadema hakuna demokrasia.

Taarifa iliyotolewa leo kwa umma na Idara ya Itikadi na Uenezi CCM, inaeleza kuwa, Kalanga amepokelewa rasmi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole usiku wa kuamkia leo.

Hivi karibuni Polepole alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa kuna wabunge wawili kutoka Chadema watahamia CCM huku akisisitiza kwamba idadi ya wanaokiomba chama hicho tawala kujiunga nacho haihesabiki.

Polepole alidai kuwa, kukosekana kwa ushirikiano kutoka uongozi wa juu wa chama ni kati ya sababu zinazowakimbiza wanaohama Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!