Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Msako wa mashine za EFD waendelea
Habari Mchanganyiko

Msako wa mashine za EFD waendelea

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema itaendelea kufanya ukaguzi wa matumizi za mashine za kutolea risiti za kielektroniki (EFD), ili kuhakikisha kila mfanyabiashara anatoa risiti za EFD na kulipa kodi stahiki. Anaripoti Regina Kelvin …. (endelea).

Hayo yalisemwa jana tarehe 31 Julai, 2018 na Kamishna wa kodi za ndani  Elijah Mwandumbya alipofanya ukaguzi wa kushtukiza katika maduka yaliyopo eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mwandumbya aliwataka wafanyabiashara kuacha kutoa sababu ya ubovu wa mashine za EFD kwa kuwa mashine hizo sasa zinafanyakazi vizuri.

“TRA  haitakubali mfanyabishara anayeonesha barua kama sababu ya kutokutoa risiti ya EFD, tatizo la mashine lilikwisha, ni wajibu wa wafanyabiashara kutoa risiti,” amesema  Mwandumbya.

Kamishna Mwandumbya amesema wafanyabiashara wote wanaostahili kutoa Risiti za EFD wanapaswa kutoa kwa kila mauzo wanayofanya kwani tatizo la mashine lilishashughulikiwa na limekwisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!