Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atoa neno zito kuondoka kwa Waitara
Habari za Siasa

Zitto atoa neno zito kuondoka kwa Waitara

Spread the love

BAADA ya Mbunge wa Ukonga (Chadema) Mwita Waitara kutangaza kurudi CCM, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe  ametoa neno kuhusu hatua hiyo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Zitto amemhoji Mwita kwa kuandika kuwa, amerudije CCM wakati viongozi waandamizi wa Chadema wana kesi mahakani  huku Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu yuko hospitalini takribani mwaka kwa majeraha ya risasi kutokana na jaribio la kuuawa.

Mbunge mwenzio yupo hospitali mwaka sasa kwa majeraha ya risasi kufuatia jaribio la kumwua. Viongozi wa Chama chako Karibu wote Ngazi ya Taifa wana kesi inayohatarisha kuwaweka jela. Watu wanauwawa na kupotea kila siku. Halafu unajiunga na hao wanaosababisha hayo? Kweli Mwita?” amehoji Zitto.

Waitara ametangaza uamuzi wa kurudi CCM mchana wa leo jijini Dar es Salaam mbele ya wanahabari baada ya kukaribishwa rasmi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Hunphrey Polepole.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!