Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga wazidi kupukutika
Michezo

Yanga wazidi kupukutika

Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya uongozi ndani ya klabu hiyo kutokana na kusambaa kwa kipande cha video kikionesha wanachama wa klabu hiyo kuhamasishana kwenda kumfanyia fujo nyumbani kwake na mapanga. Anaripoti kelvin Mwaipungu … (endelea).

Video hiyo ambayo ilikuwa ikimuonesha mwanachama maarufu wa klabu anayefahamika kwa jina la JITU kutoka tawi la Tandale akimtaka kiongozi huyo kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake, la sivyo wanachama watakwenda kumfanyia fujo nyumbani kwake.

“Nimejiuzulu rasmi nafasi yangu ya Makamu Mwemyekiti wa klabu ya Yanga, baada ya mashabiki kuhamasishana kuja nyumbani kwangu na mapanga kuja kunidhuru, najua maamuzi yangu yatawaumiza baadhi ya wanayanga kwa kuwa mimi nina familia na nisingependa kuendelea katika hali hii,” amesema Sanga.

Sanga anakuwa kiongozi wa pili kujiuzulu ndani ya klabu ya Yanga katika kipindi cha saa 48, baada ya katibu mkuu wa klabu hiyo Mkwasa kufanya hivyo siku ya jana kutokana na kusumbuliwa na maradhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!