Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga wazidi kupukutika
Michezo

Yanga wazidi kupukutika

Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya uongozi ndani ya klabu hiyo kutokana na kusambaa kwa kipande cha video kikionesha wanachama wa klabu hiyo kuhamasishana kwenda kumfanyia fujo nyumbani kwake na mapanga. Anaripoti kelvin Mwaipungu … (endelea).

Video hiyo ambayo ilikuwa ikimuonesha mwanachama maarufu wa klabu anayefahamika kwa jina la JITU kutoka tawi la Tandale akimtaka kiongozi huyo kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake, la sivyo wanachama watakwenda kumfanyia fujo nyumbani kwake.

“Nimejiuzulu rasmi nafasi yangu ya Makamu Mwemyekiti wa klabu ya Yanga, baada ya mashabiki kuhamasishana kuja nyumbani kwangu na mapanga kuja kunidhuru, najua maamuzi yangu yatawaumiza baadhi ya wanayanga kwa kuwa mimi nina familia na nisingependa kuendelea katika hali hii,” amesema Sanga.

Sanga anakuwa kiongozi wa pili kujiuzulu ndani ya klabu ya Yanga katika kipindi cha saa 48, baada ya katibu mkuu wa klabu hiyo Mkwasa kufanya hivyo siku ya jana kutokana na kusumbuliwa na maradhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!