Wednesday , 15 May 2024
Home Kitengo Michezo MO Dewji awaombea mema Yanga
Michezo

MO Dewji awaombea mema Yanga

Spread the love

MWEKEZAJI wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ amewataka wanachama na viongozi wa klabu ya Yanga kuungana upya, ili kuinusulu klabu katika kipindi hiki cha mpito ambacho kinawakabili kutokana na ukata wa fedha pamoja na wimbi la viongozi kujiuzuru. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Mo ametoa ujumbe huo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, uliosomeka: “Tunahitaji Yanga imara ambayo inaweza kushindana na Simba. Tunahitaji Yanga imara kwa ajili ya timu bora ya Taifa Stars. Ninawaombea Yanga waweze kupita katika kipindi hiki kigumu kwao, wanapaswa watulie na waungane upya.”

Kauli hiyo imekuja baada ya wachezaji wa klabu hiyo juzi kugomea mazoezi kwa kushinikiza kulipwa malimbikizo ya mishahara yao ya nyuma,  pamoja na kujiuzuru Katibu wake, Charles Mkwasa na Msemaji, Dismass Ten, huku wanachama wakitaka makamu mwenyekiti wao Clement Sanga kujiudhuru kwa kushindwa kuiongoza klabu.

Yanga imeonekana kuwa katika hali hii mbaya ya kiuchumi toka alipojiweka pembeni aliyekuwa Mwenyekiti klabu hiyo, Yusuf Manji, licha ya wanachama kumtaka arudi katika nafasi yake hiyo ya mwenyekiti katika mkutano mkuu wa klabu hiyo uliofanyika Juni 10, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Uingereza, Hispania, Italia na Ufaransa kinawaka leo

Spread the loveLIGI mbalimbali barani ulaya kuendelea leo na michezokadhaa mikali itakwenda...

Michezo

Leo mkwanja upo Meridianbet, usipishane nao

Spread the love  Siku ya leo ni nzuri sana kwa wewe mtumiaji...

Michezo

Anza wikendi yako na Meridianbet, upige mkwanja wa maana

Spread the love Siku ya leo ni nzuri sana kwa wewe mtumiaji...

Habari MchanganyikoMichezo

Arafat atoka bima na kurejea kwenye benki

Spread the loveRais wa Zanzibar Hussein Mwinyi amemteua Arafat Ally Haji kuwa...

error: Content is protected !!