Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani: China ni tishio
Kimataifa

Marekani: China ni tishio

Donald Trump
Spread the love

MAREKANI inapiga yowe kwamba, China inanyemelea nafasi yake ya kuwa taifa kubwa duniani. Inasema China inaendesha ‘vita baridi,’ pia ni tishio. Anaripoti  Yusuph Katimba…(endelea).

Akiwa kwenye semina ya masuala ya Jukwa la Ulinzi ya Aspen (Aspen Security Forum) wakati wa kipengele cha kujadili ukuaji wa China mwishoni mwa wiki, Michael Collins wa Shirika la Kijasusi la Marekani la CIA alielekeza mashambulizi yake kwa taifa hilo la Asia.

Amesema, lengo la operesheni zinazofanywa na China ni kutaka kuchukua nafasi ya Marekani kama taifa linaloongoza kwa nguvu zaidi duniani.

Collins amesema kwamba, Rais wa China Xi Jinping na serikali yake wapo wenye vita baridi dhidi ya Marekani.

Amesema kuwa, vita baridi inayopiganwa na China dhidi ya taifa lake (Marekani) haijawahi kushuhudiwa na ni tofauti na vita baridi ya awali.

“…vita baridi hii si kama ile tuliyowahi kuishuhudia wakati wa vita vya baridi,” amesema Collins na kuongeza kuwa China inatumia kila aina ya mamlaka iliyonayo iwe halali au haramu, iwe ya umma au ya kibinafsi na ya kiuchumi ama ya kijeshi ili kudhoofisha msimamo wa mpinzani wake.

“Mwisho wa siku wanataka kila nchi kote ulimwenguni, wakati wa kuamua maslahi yake juu ya masuala ya sera, wawe upande wa China na sio Marekani,” amesema.

Maoni ya Collins yamefanana na yale ya maofisa wengine wakuu wa Marekani akiwemo Mkurugenzi wa Shirika la Upelelezi la nchi hiyo (FBI), Christopher Wray na Dan Coats ambaye ni Mkurugenzi wa National Intelligence.

“Nadhani China, kwa njia nyingi inawakilisha tishio kubwa zaidi, lenye changamoto kubwa zaidi ambalo tunakabiliwa kama nchi,” amesema Wray.

Wote hao wameieleza kuwa China ni miongoni mwa nchi hatari zaidi kwa taifa la Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!