Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nondo ‘awaponza’ Sirro, AG na DCI
Habari za SiasaTangulizi

Nondo ‘awaponza’ Sirro, AG na DCI

Spread the love

MAWAKILI wanaomwakilisha Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP), Abdul Nondo wamefungulia kesi Mkuu wa jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya Jinai (DCI), Mwasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa kumshikilia kwa zaidi ya saa 48 mwanafunzi huyo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Nondo alitoweka jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia Machi 8, mwaka huu kabla ya kupatikana wilayani Mafinga, Iringa ambapo alidai kuzinduka na kujikuta eneo hilo baada ya kutekwa na watu wasiofahamika. Hata hibyo taarifa ya Jeshi la Polisi imedai kuwa kijana huyo hakutekwa bali alienda mkoani humo kumtembelea mpenzi wake.

Tangu tarehe 8 Machi mwaka huu, polisi wanamshikilia mwanafunzi huyo, ikiwa ni zaidi ya siku 11 sasa. Awali alisafirishwa kutoka Iringa mpaka Dar lakini haijajulikana amehifadhiwa katika kituo gani cha polisi huku mawakili na ndugu zake wakidai kuzuiwa kumuona kwa kipindi hicho chote.

Mawakili wa mtandao huo wakiongozwa na Jebra Kambole, Jones Sendodo na Reginald Martine wamefungua shauri la kumtaka IGP, AG na DCI wajieleze kwanini wanaendelea kumshikilia Nondo, na kisha wamuachie kwa dhamana kijana huyo au wamfikishe mahakamani haraka, hilo kwenye mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam kushinikiza kufikishwa mahakamani kwa Nondo.

Wakili Jones Sendodo ameiambia MwanaHALISI Online ameeleza kuwa kesi hiyo imeshafunguliwa na imepangiwa Jaji na kwamba itasikilizwa Tarehe 21 Machi.

Wakili Sendodo amesema kuwa Jeshi la Polisi linatakiwa limmpeleke mahakamani Nondo ili kumshtaki kwa mashtaka wanayoyadai au wamuachie kwa dhamana ya polisi kama bado hawajakamilisha upelelezi.

“Polisi wanaendelea kumshikilia ilihali sisi mawakili wake hawaturuhusu tumuone.”

Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambasasa aliripotiwa hivi karibuni akisema kuwa bado wanaendelea na upelelezi kwenye kesi hiyo na kwamba watamfikisha mahakamani upelelezi ukikamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!