JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limeridhia kujiuzuru kwa Mwenyekiti wake Theophil Makunga aliyeomba kujiuzulu. Anaripoti Angel Willium … (endelea).
Makunga aliomba kujiuzulu jana Ijumaa kwa kuuandikia uongozi wa jukwaa hilo.
Kutokana na uamuzi huo wa Makunga, TEF walikutana katika mkutano wa dharura na kuridhia barua yake.
Katika ujumbe uliosambazwa na TEF na kusainiwa na Katibu wake, Neville Meena, umeeleza kujiuzulu kwa aliyekuwa mwenyekiti wake watakosa busara zake ambazo bado zilikuwa zinahitajika katika ukuaji wa taasisi hiyo.
TEF inamtakia kila la kheri Makunga katika majukumu yake mengine.
Leave a comment