Friday , 3 May 2024
Habari za Siasa

UVCCM wamkera Msigwa

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM), Kheri James
Spread the love

MBUNGE wa Iringa Mjini Peter Msigwa ameshangazwa na kibwagizo kilichokuwa kikitumiwa na vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha kusema upinzani unakufa, kwenye mkutano wa tisa wa UVCCM Taifa uliofanyika siku mbili katika ukumbi wa Chuo Cha Mipango, Dodoma, anaandika Shabani Matutu.

Katika mkutano huo ambao uliwachagua viongozi wao wapya akiwemo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM, Kheri James walikuwa wakitumia kibwagizo kinachosema kwamba ‘upinzani unakufa’ jambo lililomkera Msigwa.

Msigwa alisema “Fine! tukubaliane Kuwa upinzani unakufa! Jambo la kujiuliza hivi upinzani ukifa upinzani zitaongezeka ajira ngapi! Umaskini utapungua kwa kiwango gani? Haki za binadamu zitalindwa kwa kiwango gani?

Anaongeza kuwa, “tujiulize utawala bora utaimarika kwa kiwango gani? Demokrasia itaimarishwa kwa kiwango gani? Uhuru wa kutoa mawazo na vyombo vya habari utaimarika kwa kiwango gani! Wanatakiwa watambue kuwa haya yote hayana chama.”

Mbunge huyo alisema kwamba mategemeo yake alitarajia CCM wangeutumia mkutano huo kwa kuleta majibu ya masuala hayo muhimu ambayo kila mwananchi angependa kuona majibu yake kwa vitendo.

Wengine waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Tabia Mwita aliyechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa UVCCM na viongozi wengine waliotangazwa katika mkutano huo ni wajumbe wa Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu wa UVCCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!