Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwenyekiti UVCCM arudishwa rumande
Habari za SiasaTangulizi

Mwenyekiti UVCCM arudishwa rumande

Spread the love

BAADA ya kukamatwa, Sadifa Khamis ambaye ni Mwenyekiti wa UVCCM Taifa leo amefikishwa mahakamani Dodoma kwa tuhuma za kugawa rushwa, anaandika Hamis Mguta.

Mwenyekiti huyo amerudishwa rumande mpaka Desemba 19 mwaka 2017 akituhumiwa kuwapa wajumbe soda na nauli.

Awali Sadifa pamoja na mjumbe mmoja wa UVCCM waliwekwa sero jana kwa tuhuma za kutoa na kupokeea rushwa kwa ajili ya kununua uongozi na leo .

Kitendo cha Sadifa kutuhumiwa, kimenukuliwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dk John Magufuli kama ni jambo la aibu ambapo alisema kijana ambaye ana kashfa ya rushwa hasipatiwe nafasi yoyote ndani ya uongozi wa vijana kwa maana hawawezi kuwa watenda kazi wema ndani ya jumuiya hiyo.

Mbali na Rais Magufuli kukerwa na vitendo vya rushwa pia ametangaza kuifuta bodi ya UVCCM kwa maelezo kuwa haina msaada wowote kwa jumuiya hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!