Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa UVCCM wamkera Rais Magufuli kwa rushwa
Habari za Siasa

UVCCM wamkera Rais Magufuli kwa rushwa

Rais John Magufuli alipokuwa anaomba kura
Spread the love

LICHA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kujipambanua kuwa kinapambana na vitendo vya rushwa na ufisadi, bado baadhi ya  jumuiya ndani ya chama hicho ziimeonekana kukumbwa na kashifa ya rushwa na ufisadi wa kutisha, anaandika Dany Tibason.

Hali hiyo ya baadhi ya jumuiya kukumbwa na kashifa ya rushwa, imeooneekana kumtisha na kumkera mwenyekiti wa CCM Taifa, John Pombe Magufuli.

Akifungua Mkutano wa tisa wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) ambao pia unaambatana na uchaguzi wa viongozi kwa ngazi ya taifa Rais Magufuli amesema amesikitishwa na kuwepo kwa vitendo vya kwa baadhi ya viongozi ndani ya jumuiya hiyo.

Muda mfupi wakati akifungua mkutano huo Rais Magufuli amesema licha ya chama hicho kupambana na rushwa na ufisadi lakini mwenyekiti wa UVCCM Taifa Sadifa…. pamoja na mjumbe mmoja wapo sero kwa tuhuma za kutoa na kupokeea rushwa kwa ajili ya kununua uongozi.

Mwenyekiti wa CCCM Taifa amesema ni jambo la aibu kwa vijana wa CCM kukumbwa ba kashifa la rushwa na kuwaelekeza vijana kutowapatia nafasi vijana ambao wanaonekana kutuhumiwa kwa kutoa au kupokea rushwa.

Amesema kijana ambaye ana kashfa ya rushwa hasipatiwe nafasi yoyote ndani ya uongozi wa vijana kwa maana hawawezi kuwa watenda kazi wema ndani ya jumuiya hiyo.

Mbali na Rais Magufuli kukerwa na vitendo vya rushwa pia ametangaza kuifuta bodi ya UVCCM kwa maelezo kuwa haina msaada wowote kwa jumuiya hiyo.

Amesema vijana wana miradi mingi lakini bado kuna wajanja wachache ambao wamekuwa wakijichotea hela kwa ajili ya kujinufaisha badala ya vijana kunufaika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!