Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ukawa watangaza vita na NEC uchaguzi wabunge
Habari za SiasaTangulizi

Ukawa watangaza vita na NEC uchaguzi wabunge

Spread the love

VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuahirisha uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 13, 2018 vinginevyo havitashiriki, anaandika Faki Sosi.

Vyama hivyo ni Chadema, CUF, Chauma, NLD na NCCR-Mageuzi.

Akizungumza kwa niaba ya Ukawa leo Jumatatu Desemba 11 ,2017, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema vyama hivyo havitashiriki uchaguzi kwa sababu ya kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata 43 uliofanyika Novemba 26,2017.

Mbowe amesema uchaguzi huo uligeuka kuwa uwanja wa vita badala ya kuwa jukwaa la kuchagua viongozi.

“Ndiyo maana tunaiomba Serikali kuahirisha uchaguzi ili wadau wajadili kasoro zilizojitokeza,” amesema.

Amesema majadiliano ya wadau yatasaidia kuondoa kasoro zilizojitokeza, hivyo kuwa na uchaguzi ulio huru na haki.
Mbowe amesema iwapo Serikali kupitia NEC itakataa kuahirisha uchaguzi wao hawatashiriki.

“Hatuwezi kushiriki uchaguzi wakati tumefungwa mikono, hii ni sawa na timu ya mpira kwenda kwenye mashindano bila kufanya mazoezi,” amesema.

Mbowe amesema wakati vyama vya upinzani vikizuiwa kufanya mikutano ya hadhara, chama tawala kinafanya mikutano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!