Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nassari ‘ashambuliwa’ kwa risasi
Habari za SiasaTangulizi

Nassari ‘ashambuliwa’ kwa risasi

Joshua Nassari, Mbunge wa Arumeru Mashariki. Picha ndogo maganda ya risasi zilizotumika kufanya katika shambulio hilo
Spread the love

MAKUMI ya watu wenye silaha, jana usiku wakiwa na bunduki na risasi za moto, walivamia nyumbani kwa mbunge wa Chadema katika jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, kwa lengo la kufanya mauaji, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa kutoka mjini Arusha zinasema, watu hao wenye silaha, walivamia nyumbani kwa mbunge huyo, maeneo ya Usa River, majira ya saa tano na nusu usiku wa kuamkia leo Jumamosi.

Kwa mujibu wa Nassari, wakati “watu hao wasiojulikana” walivamia nyumbani kwake, muda mfupi baada ya yeye kurejea kutoka chuo cha MSTCDC (Danish), ambako alikwenda kuhudhuria mafunzo ya uongozi kwa vijana.

https://twitter.com/joshua_nassari/status/936733889405640704

“Hawa watu wameruka uzio wa nyumba yangu na kuingia ndani. Walipoingia ndani, walikutana na mbwa na wakaamua kumfyatua risasi kadhaa na kumuua,” ameeleza mbunge huyo mahiri wa Arumeru Mashariki.

Anasema, baada ya watu hao kuingia ndani na kuanza kufyatua risasi, yeye na mkewe walifanikiwa kutoroka kupitia mlango wa uani, kabla ya kuripoti tukio hilo kituo cha Polisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!