Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Michezo Diamond Platnumz ambwaga Mobeto mahakamani
Michezo

Diamond Platnumz ambwaga Mobeto mahakamani

Picha kubwa Hamisa Mobeto. Ndogo kulia mtoto wake Prince Abdul aliyezaa na Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz (kushoto)
Spread the love

MSANII Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemgalagaza mzazi mwenzake, Mwanamitindo Hamisa Mabeto katika kesi ya madai aliyoifungua katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kudai matunzo ya mtoto Prince Abdul, anaandika Angel Willium.

Hakimu Devotha Kisoka wa Mahakama hiyo ametupilia mbali madai ya Mobeto katika kesi hiyo baada ya kusikiliza hoja za pande hizo mbili husika.

Diamond aliwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto akidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi. Hoja ambayo ilipingwa na Mobeto.

Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine anaiomba matunzo ya mtoto waliozaa na msanii Diamond.

Mwanamitindo huyo pia anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi na alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys.

Kupitia hati hiyo ya madai, Mobeto anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.

Diamond aliwasilisha hati ya majibu hayo kinzani akipinga maombi hayo ya Mobeto akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi ya Tsh. 5 milioni kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!