Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco
Habari Mchanganyiko

Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco

Waziri wa Nishati na Madini, Merdad Karemani
Spread the love

WAZIRI wa Nishati na Madini, Merdad Karemani amemtoa  ‘kafara’ meneja uendeshaji wa mtambo wa kufua umeme wa Kidatu mkoani Morogoro kufuatia nchi kuingia gizani mara kwa mara kwa kukosa umeme kuanzia jana, anaandika Hamis Mguta.

Amefanya maamuzi ya kumtimua mtumishi kazi mtumishi huyo wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), leo alipofanya ziara katika gridi ya taifa eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam.

Karemani, katika ziara hiyo amemtaka Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Abdallah Ikwasa kumuondoa kazini mtumishi huyo kwa madai kwamba amekuwa mzembe.

 “Leo meneja wa Kidatu sitaki kumsikia akiwa kwenye kazi nataka kuona nani umemuweka, lakini aondoke kwanza, na wewe protection nimekupa siku tatu kuhakikisha unarekebisha mfumo wako, tunataka mtuambie nini kimetokea nini tuzuie ili kisitokee, hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea, huwezi ondoka na nawaambia leo umeme ukizimika nataka kukuta barua nyie wenyewe mmeacha kazi” amesema.

Tazama Video hapo chini…..

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!