Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Hukumu ya Sheikh Ponda yakwama
Habari za SiasaTangulizi

Hukumu ya Sheikh Ponda yakwama

Sheikh Ponda Issa Ponda
Spread the love

MAHAKAMA ya Rufaa imeshindwa kutoa hukumu ya rufaa ya Serikali dhidi ya Sheikh Issa Ponda baada ya jaji kutokamilisha kuiandika, anaandika Faki Sosi.

Katika rufaa hiyo Serikali inapinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro iliyomuachia huru Sheikh Ponda katika tuhuma ya uchochezi.

Hukumu hiyo iliyitarajiwa kutolewa leo na Jaji Mkasi Mongwa ambaye amesema ameshindwa kutoa hukumua hiyo kwa kuwa hajamaliza kuianda na badala yake ataitoa Tarehe 16 Novemba mwaka huu.

Inatarajiwa kwenye hukumu hiyo endapo Jaji Mongwa anayesikiliza shauri hilo ataridhika na madai ya upande wa Serikali, Sheikh Ponda atatiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu.

Kama Jaji hataona ukweli katika madai ya Serikali, atatupilia mbali rufaa hiyo na kumuachia huru Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!