Sunday , 3 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Mvua zaleta balaa Dar, Pwani
Habari Mchanganyiko

Mvua zaleta balaa Dar, Pwani

Daraja la Kiluvya
Spread the love

MVUA zinazoendelea kunyesha kuanzia jana mchana zimeanza kuleta madhara baada ya daraja la Kiluvya linalounganisha mkoa wa Pwani na Dar es Salaam kukatika.

Kutokana na daraja hilo kukatika hudumza za usafiri  wa magari ya abiria, mizigo na binafsi umesitishwa na wananchi wameombwa kutumia barabara ya Bagamoyo.

Daraja hilo ni kiungo muhimu kati ya jiji la Dar es Salaam pamoja na mikoa mbalimbali ya Kaskazini, Kati, Kanda ya Ziwa,  Nyanda za juu Magharibu.

Daraja la Kiluvya

Aidha, mvua hizo zimesababisha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam yamejaa maji zikiwamo nyumba na kusababisha uharibifu wa mali.

Adha daraja lingine eneo la Mbezi beach jijini Dar es Salaam ‘maarufu la Jeshi’  kutokea Kawe limejaa maji na inadaiwa magari kadhaa yamezama na njia imefungwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Habari Mchanganyiko

TARURA kujenga madaraja 189 kwa teknolojia ya mawe

Spread the loveWakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imejipanga kujenga...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

error: Content is protected !!