Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco
Habari Mchanganyiko

Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco

Waziri wa Nishati na Madini, Merdad Karemani
Spread the love

WAZIRI wa Nishati na Madini, Merdad Karemani amemtoa  ‘kafara’ meneja uendeshaji wa mtambo wa kufua umeme wa Kidatu mkoani Morogoro kufuatia nchi kuingia gizani mara kwa mara kwa kukosa umeme kuanzia jana, anaandika Hamis Mguta.

Amefanya maamuzi ya kumtimua mtumishi kazi mtumishi huyo wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), leo alipofanya ziara katika gridi ya taifa eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam.

Karemani, katika ziara hiyo amemtaka Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Abdallah Ikwasa kumuondoa kazini mtumishi huyo kwa madai kwamba amekuwa mzembe.

 “Leo meneja wa Kidatu sitaki kumsikia akiwa kwenye kazi nataka kuona nani umemuweka, lakini aondoke kwanza, na wewe protection nimekupa siku tatu kuhakikisha unarekebisha mfumo wako, tunataka mtuambie nini kimetokea nini tuzuie ili kisitokee, hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea, huwezi ondoka na nawaambia leo umeme ukizimika nataka kukuta barua nyie wenyewe mmeacha kazi” amesema.

Tazama Video hapo chini…..

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!