Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari
Habari za SiasaTangulizi

Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Spread the love

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemugeuzia kibao Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  (Chadema)  ambaye amewapelekea ushahidi wa namna Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alivyotumia rushwa kuwashawishi Madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukihama chama hicho, anaandika mwandishi wetu.

Tofauti na ilivyotarajiwa na wengi kwamba  taasisi hiyo ingeufanyia kazi ushahidi uliowasilishwa kwao na Mbunge huyo, lakini leo imemuonya mwanasiasa huyo na kumtaka asitoe aina yoyote ya shinikizo baada ya kuwapa ushahidi.

“Hii Taasisi haishinikizwi na mtu yeyote na hapaswi hata mara moja kutushinikiza…. natoa onyo jingine, endapo ataendelea na utaratibu huu tutachukua hatua za kisheria dhidi  yake”

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola, ametoa onyo hilo leo na kusisitiza kuwa hawafanyi kazi kwa shinikizo la mtu.

Nassari akiongozana na wabunge kadhaa wa Chadema wameiwasilisha ushahidi huo wa video kwa TAKUKURU ili iweze kufanya uchunguzi wake kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!