Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Switzerland yawakumbuka walemavu
Habari Mchanganyiko

Switzerland yawakumbuka walemavu

Spread the love

WATU wenye ulemavu nchini wameiomba serikali  na taasisi mbalimbali binafsi kuwasaidia  eneo la   kujenga ofisi ya kudumu. Anaandika Angela Willium

Wamesema wanahitaji ofisi kwa kuwa hivi sasa sehemu wanayotumia wameazimwa kwa muda na Msikiti wa Membe Chai uliopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,  Mwenyekiti wa Taasisi  ya Walemavu ijulikanayo kama MITWE, Habibu Hamimu amesema tatizo hilo la kukosa ofisi wamekuwa nalo kwa muda mrefu sasa.

Aliyasema hayo wakati akipokea msaada wa viti vya walemavu na baiskeli kutoka Taasisi ya Furaha ya Switzerland.

“Tunaiomba serikali na wana  jamii watusadie eneo la kujenga ofisi ya kudumu  kwani hapa tulipo ni jengo la Msikiti wa   Mwembechai ambayo hata hivyo  hiyo inavuja kipindi cha mvua na misaada tuyopokea ni mikubwa ikilinganisha na ofisi tuliyo nayo, ” amesema Hamimu

Kwa upande wake, Katibu wa chama hicho  wilaya ya Kinondoni,   Saidi Machaku amesema walemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo suala la afya.

“Wazazi au walezi wanao ishi na watu wenye ulemavu tuna waomba muwe mna waleta walemavu wenzetu katika kupokea misaada badala ya kuwafungia ndani na hapa kuna mlemavu mmoja sijamuona nahisi wazazi hawajamleta kwa kuwa wanaona aibu kuja naye, ” amelalamika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

error: Content is protected !!