Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari
Habari za SiasaTangulizi

Takukururu yamgeuzia kibao Mbunge Nassari

Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Spread the love

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemugeuzia kibao Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  (Chadema)  ambaye amewapelekea ushahidi wa namna Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alivyotumia rushwa kuwashawishi Madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kukihama chama hicho, anaandika mwandishi wetu.

Tofauti na ilivyotarajiwa na wengi kwamba  taasisi hiyo ingeufanyia kazi ushahidi uliowasilishwa kwao na Mbunge huyo, lakini leo imemuonya mwanasiasa huyo na kumtaka asitoe aina yoyote ya shinikizo baada ya kuwapa ushahidi.

“Hii Taasisi haishinikizwi na mtu yeyote na hapaswi hata mara moja kutushinikiza…. natoa onyo jingine, endapo ataendelea na utaratibu huu tutachukua hatua za kisheria dhidi  yake”

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Valentino Mlowola, ametoa onyo hilo leo na kusisitiza kuwa hawafanyi kazi kwa shinikizo la mtu.

Nassari akiongozana na wabunge kadhaa wa Chadema wameiwasilisha ushahidi huo wa video kwa TAKUKURU ili iweze kufanya uchunguzi wake kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mobhare Matinyi Msemaji mpya wa Serikali

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mkuu wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the loveBasi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni...

error: Content is protected !!