Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mzimu wa Bashite wazidi kupapasa
Habari za SiasaTangulizi

Mzimu wa Bashite wazidi kupapasa

Boniface Jacob, Meya wa Ubungo. Picha ndogo, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

MEYA wa Manspaa ya Ubungo, Bonface Jacob amesema anakabiliwa vitisho na vishawishi mbalimbali ili kuhakikisha anafuta kesi aliyoifungua dhidi ya Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ya kughushi vyeti, anaandika Faki Sosi.

Makonda anatuhumiwa kudanganya na kutumia vyeti ambavyo siyo vya kwake, na kwamba yeye jina lake alilopewa na wazazi wake ni ‘Bashite’

Hata hivyo, hakuweka bayana anapokea vitisho kutoka kwa nani pamoja.

Akizungumza na vyombo vya habari muda mfupi baada ya kutoka kwenye ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma amesema kuwa Mkuu wa Mkoa huyo amekiuka sheria za utumishi wa umma.

“Nimemfungulia shuri la kughushi vyeti pamoja na kula kiapo mbele ya Rais kuwa Mkuu wa mkoa wakati akijua jina siyo la kwake ambalo sio la kwake kinyume cha sheria ya viongozi na watumishi wa umma”, amesema Jacob.

Amesema kuwa tayari kuna viashiria vya ushawishi kutoka kwa watu wa Makonda wanaotaka akubali kuondoa shauri hilo.

Ametaja vitisho anavyokabiliana navyo ni pamoja na kusingiziwa kwamba anatumia ofisi kufanya mikutano ya kisiasa.
Fuatilia Video Chini kujua kilichozungumzwa na Meya Boniface Jacob

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

error: Content is protected !!