Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Sakata la ‘Bashite’ kutolewa maelezo kesho
Habari Mchanganyiko

Sakata la ‘Bashite’ kutolewa maelezo kesho

Spread the love

TUME  ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inatarajia kumhoji Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob kuhusu  madai yake aliyowasilisha kwa tume hiyo akitaka Mkuu wa  Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwamba ameghushi vyeti vya shule, anaandika Faki Sosi.

Jacob amesema kuwa tume hiyo imemtaka afike ofisini kwao kesho asubuhi ili aweze kutoa maelezo juu ya mashtaka yake juu ya Makonda.

Meya huyo ambaye pia ni Diwani wa Ubungo amesema ameitwa kupitia barua yenye kumbukumbu namba  CAG 31/37/01/42.

Hata hivyo, Jacob amesema kuwa tayari kuna viashiria vya vishawishi vya yeye kuachana na shauri hilo linalomkabili Makonda.

Mwezi Machi mwaka huu  Jacob aliwasilisha mashtaka manne katika tume hiyo pamoja na moja la  jinai ambalo ni la kughushi  vyeti vya taaluma.

Hivi karibuni Makonda alipachikwa jina la Bashite ambalo linadaiwa ndilo jina lake halisi alilopewa na wazazi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!