Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha
Habari Mchanganyiko

Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha

Samson Petro kijana aliyeuwawa na Polisi. Picha ndogo Kamanda wa Arusha, Charles Mkumb
Spread the love

MTUHUMIWA aliyekuwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kuhusika na utekaji na mauaji ya watoto wawili Maureen na Ikram amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kutoroka mikononi mwa polisi, anaandika Irene David.

Kijana huyo anayejulikana kwa jina la Samson Petro, alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya utekaji wa watoto katika mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha na Geita kwa lengo la kujipatia fedha.

Samson alipigwa risasi wakati akijaribu kutoroka kituo cha polisi na mwili wake upo katika hospitali ya mkoa wa Arusha Mount Meru.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo , amekiri kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa alipigwa risasi baada ya kujaribu kuwakimbia polisi alipokuwa amepelekwa kuwaonyesha mtu anayedaiwa kuwa walikuwa wanashirikiana katika utekaji huo wa watoto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!