Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha
Habari Mchanganyiko

Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha

Samson Petro kijana aliyeuwawa na Polisi. Picha ndogo Kamanda wa Arusha, Charles Mkumb
Spread the love

MTUHUMIWA aliyekuwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kuhusika na utekaji na mauaji ya watoto wawili Maureen na Ikram amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kutoroka mikononi mwa polisi, anaandika Irene David.

Kijana huyo anayejulikana kwa jina la Samson Petro, alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya utekaji wa watoto katika mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha na Geita kwa lengo la kujipatia fedha.

Samson alipigwa risasi wakati akijaribu kutoroka kituo cha polisi na mwili wake upo katika hospitali ya mkoa wa Arusha Mount Meru.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo , amekiri kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa alipigwa risasi baada ya kujaribu kuwakimbia polisi alipokuwa amepelekwa kuwaonyesha mtu anayedaiwa kuwa walikuwa wanashirikiana katika utekaji huo wa watoto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!