
Samson Petro kijana aliyeuwawa na Polisi. Picha ndogo Kamanda wa Arusha, Charles Mkumb
MTUHUMIWA aliyekuwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kuhusika na utekaji na mauaji ya watoto wawili Maureen na Ikram amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kutoroka mikononi mwa polisi, anaandika Irene David.
Kijana huyo anayejulikana kwa jina la Samson Petro, alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya utekaji wa watoto katika mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha na Geita kwa lengo la kujipatia fedha.
Samson alipigwa risasi wakati akijaribu kutoroka kituo cha polisi na mwili wake upo katika hospitali ya mkoa wa Arusha Mount Meru.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo , amekiri kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa alipigwa risasi baada ya kujaribu kuwakimbia polisi alipokuwa amepelekwa kuwaonyesha mtu anayedaiwa kuwa walikuwa wanashirikiana katika utekaji huo wa watoto.
More Stories
Wanafunzi walilia madarasa Mtwara, Silinde awajibu
LSF, NGO’s zajadili mfumo upatikanaji haki Tanzania
Majaliwa atoa maagizo kwa wazazi, walezi