Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

HATMA ya kesi ya mbunge wa Ubunge, Saed Kubenea (Chadema) inatarajiwa kujulikana kesho, anaandika Dany Tibason.

Kesho Mahakama ya Wilaya ya Dodoma itaamua ama itaendelea kuipiga kalenda kesi hiyo, kufutwa ama kusikilizwa.

Kwa mujibu wa Hakimu wa mahakama hiyo, James Karayemaha kesi hiyo itatajwa kesho baada ya leo Wakili wa serikali, Lina Magoma, kueleza kuwa kuna mambo mbalimbali ambayo yana mapungufu katika jarada la kesi ambayo inamkabili mbunge huyo.

Kubenea anashtakiwa kwa kosa la jinai ambalo anadaiwa kumshambulia mbunge wa viti maalum (CCM), Juliana Shonza wakati wa bunge la bajeti.

Hakimu James Karayemaha alipanga tarehe hiyo na wakili wa serikali, Lina Magoma, alikubaliana naye hivyo kesi hiyo itaendelea Septemba 5, mwaka huu.

Awali Kubenea alisema utaratibu wa kisheria uliotumika siyo mzuri hivyo ni vyema kesi hiyo ingebaki polisi hadi hapo upepelezi utakapokamilika na kwamba ni matumizi mabaya ya raslmali za serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!