Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

HATMA ya kesi ya mbunge wa Ubunge, Saed Kubenea (Chadema) inatarajiwa kujulikana kesho, anaandika Dany Tibason.

Kesho Mahakama ya Wilaya ya Dodoma itaamua ama itaendelea kuipiga kalenda kesi hiyo, kufutwa ama kusikilizwa.

Kwa mujibu wa Hakimu wa mahakama hiyo, James Karayemaha kesi hiyo itatajwa kesho baada ya leo Wakili wa serikali, Lina Magoma, kueleza kuwa kuna mambo mbalimbali ambayo yana mapungufu katika jarada la kesi ambayo inamkabili mbunge huyo.

Kubenea anashtakiwa kwa kosa la jinai ambalo anadaiwa kumshambulia mbunge wa viti maalum (CCM), Juliana Shonza wakati wa bunge la bajeti.

Hakimu James Karayemaha alipanga tarehe hiyo na wakili wa serikali, Lina Magoma, alikubaliana naye hivyo kesi hiyo itaendelea Septemba 5, mwaka huu.

Awali Kubenea alisema utaratibu wa kisheria uliotumika siyo mzuri hivyo ni vyema kesi hiyo ingebaki polisi hadi hapo upepelezi utakapokamilika na kwamba ni matumizi mabaya ya raslmali za serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!