Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Kubenea yazidi kupigwa kalenda

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

HATMA ya kesi ya mbunge wa Ubunge, Saed Kubenea (Chadema) inatarajiwa kujulikana kesho, anaandika Dany Tibason.

Kesho Mahakama ya Wilaya ya Dodoma itaamua ama itaendelea kuipiga kalenda kesi hiyo, kufutwa ama kusikilizwa.

Kwa mujibu wa Hakimu wa mahakama hiyo, James Karayemaha kesi hiyo itatajwa kesho baada ya leo Wakili wa serikali, Lina Magoma, kueleza kuwa kuna mambo mbalimbali ambayo yana mapungufu katika jarada la kesi ambayo inamkabili mbunge huyo.

Kubenea anashtakiwa kwa kosa la jinai ambalo anadaiwa kumshambulia mbunge wa viti maalum (CCM), Juliana Shonza wakati wa bunge la bajeti.

Hakimu James Karayemaha alipanga tarehe hiyo na wakili wa serikali, Lina Magoma, alikubaliana naye hivyo kesi hiyo itaendelea Septemba 5, mwaka huu.

Awali Kubenea alisema utaratibu wa kisheria uliotumika siyo mzuri hivyo ni vyema kesi hiyo ingebaki polisi hadi hapo upepelezi utakapokamilika na kwamba ni matumizi mabaya ya raslmali za serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!