Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hoja ya Bombadier kupasua Bunge kesho
Habari za Siasa

Hoja ya Bombadier kupasua Bunge kesho

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Bombadier
Spread the love

HOFU  imetanda kuhusu mkutano wa Bunge unaotarajia kuanza kesho kwamba unaweza kutekwa na sakata la kukamatwa ndege ya serikali aina ya Bombadier, anaandika  Dany Tibason, Dodoma. 

Wabunge wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameanza kuingiwa na hofu na kwamba kuna uwezekano wabunge wa upinzani wakaibuka na kutaka majibu ya serikali kuhusu sakata la ndege hiyo.

Wakizungumza kwa mashariti ya kutokutajwa majina wabunge hao wa CCM wamesema  kama Spika wa Bunge, Naibu Spika au wenyeviti hawatakuwa wakali kuzuia hoja hizo Bunge linaweza kuwaka moto.

Baadhi ya wabunge kutoka mikoa ya kanda ya ziwa wamesema kuwa awali wawakilishi hao walisifu kitendo cha rais John Magufuli kuzui mchanga wa makenikia lakini hili la  Bombadier linaweza kuleta shida.

Wamesema Bunge linaweza kutawaliwa na mijadala ambayo inaweza kutokana na upinzani kutaka majibu ya haraka kuhusu sakata la Makinikia, kikao cha majadiliano na wawakilishi wa kampuni ya Barrick waliokuja nchini kuzungumza na sekali pamoja na ndege ya Bombadier.

Amesema kwa sasa wabunge wengi wa CCM ni kama wameisha kata tamaa ya kuendelea kumtetea rais kwa kuwa mambo mengi ambayo yanaibuliwa na wapinzani mengi yanaonekana kuwa ni ya kweli licha ya kupindisha ukweli.

“Kwanza kwa sasa tumeisha tofautiana wabunge wengi hatuana kauli moja wabunge wengine wamekuwa waoga kuongea ukweli kilichobaki ni kulalamikiana,” amesema

Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) amesema Bunge linaloanza kesho kuna uwezekana likatawaliwa na hoja ambazo zinalenga kujua mstakabari wa taifa.

Kubenea ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kutoka mahakamani ambapo anakabiliwa na kesi ya kudaiwa kumshambulia mbunge mwenziwe wa CCM.

Hivi karibuni mwanasheria mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu  amesema ataingia bungeni na hoja mbalimbali ikiwamo hiyo ya kukamatwa ndege ya serikali nchini Canada.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!