Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Hakimu ataka serikali iharakishe upelelezi kesi ya Manji
Habari Mchanganyiko

Hakimu ataka serikali iharakishe upelelezi kesi ya Manji

Yusuph Manji, akizungumza na Wakili wake Hudson Ndusyepo
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeuitaka Jamhuri kukamilisha upelelezi wa kesi ya uhujumu uchimi inayomkabili mfanyabiashara Yusuf Manji, anaandika Faki Sosi.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba amesema kuwa upande wa mashtaka upelelezi ukamilishwe haraka ili matokeo ya kesi hiyo yajulikane.

Leo mahakamani hapo wakili wa serikali, Wankyo Simon aliomba tarehe ya kutajwa kwa kesi hiyo na kwamba upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Hata hivyo wakili utetezi aliutaka upande wa Serikali kueleza hatua waliyofika kwenye upelelezi huo. Kesi hiyo imeaihirishwa mpaka Agosti 31 mwaka huu.

Awali mfanyabiashara huo alisomewa mashtaka manane akiwa amelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Manji (41) na wenzake, wanadaiwa kukutwa na vitambaa vyenye thamani ya Sh200 milioni, vinavyotumika kutengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Pia, wanadaiwa kukutwa na mihuri.

Wanashtakiwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi na Sheria ya Usalama wa Taifa. Washtakiwa wengine ni Deogratius Kisinda (28), Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43).

Walisomewa mashtaka hayo ndani ya wodi aliyolazwa Manji na wakati yakisomwa, Manji alikuwa amevaa sare za bluu za wagonjwa na alikuwa ameketi kitandani huku mkononi akiwa ametundukiwa dripu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!