Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Hakimu ataka serikali iharakishe upelelezi kesi ya Manji
Habari Mchanganyiko

Hakimu ataka serikali iharakishe upelelezi kesi ya Manji

Yusuph Manji, akizungumza na Wakili wake Hudson Ndusyepo
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeuitaka Jamhuri kukamilisha upelelezi wa kesi ya uhujumu uchimi inayomkabili mfanyabiashara Yusuf Manji, anaandika Faki Sosi.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba amesema kuwa upande wa mashtaka upelelezi ukamilishwe haraka ili matokeo ya kesi hiyo yajulikane.

Leo mahakamani hapo wakili wa serikali, Wankyo Simon aliomba tarehe ya kutajwa kwa kesi hiyo na kwamba upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Hata hivyo wakili utetezi aliutaka upande wa Serikali kueleza hatua waliyofika kwenye upelelezi huo. Kesi hiyo imeaihirishwa mpaka Agosti 31 mwaka huu.

Awali mfanyabiashara huo alisomewa mashtaka manane akiwa amelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Manji (41) na wenzake, wanadaiwa kukutwa na vitambaa vyenye thamani ya Sh200 milioni, vinavyotumika kutengeneza sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Pia, wanadaiwa kukutwa na mihuri.

Wanashtakiwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi na Sheria ya Usalama wa Taifa. Washtakiwa wengine ni Deogratius Kisinda (28), Abdallah Sangey (46) na Thobias Fwere (43).

Walisomewa mashtaka hayo ndani ya wodi aliyolazwa Manji na wakati yakisomwa, Manji alikuwa amevaa sare za bluu za wagonjwa na alikuwa ameketi kitandani huku mkononi akiwa ametundukiwa dripu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!