Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mmiliki wa Samsung duniani atupwa jela
Kimataifa

Mmiliki wa Samsung duniani atupwa jela

Lee Jae-yong aliyetarajia kurithi kampuni ya Samsung, akiwa chini ya ulinzi baada ya kuhukumiwa
Spread the love

MRITHI aliyetarajia kurithi kampuni ya Samsung, Lee Jae-yong amehukumiwa kifungo cha miaka mitano na mahakama ya nchini Korea Kusini kwa kosa la rushwa, anaandika Jovina Patrick.

Lee ambaye pia anafahamika kama Jay Y Lee na kiongozi wa kampuni hiyo kubwa zaidi ya kutengeneza simu duniani, amekuwa kizuizini tangu mwezi februari akikabiliwa na tuhuma kadhaa za rushwa.

Miongoni mwa makosa aliyokabiliwa nayo ni utoaji rushwa, wizi wa mali ya umma na kuficha mali nje ya nchi.

Wakili wa Lee amesema watakata rufaa kupinga uamuzi uliotolewa na mahakama hiyo,”Tuna imani kwamba hukumu hii itabatilishwa,” wakili Song Wu-cheol amewaambia wanahabari baada ya kusomwa kwa hukumu hiyo.

Hata hivyo, uamuzi huo wa mahakama ni pigo kubwa kwa kampuni hiyo kubwa zaidi na inayofahamika zaidi duniani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!