Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mmiliki wa Samsung duniani atupwa jela
Kimataifa

Mmiliki wa Samsung duniani atupwa jela

Lee Jae-yong aliyetarajia kurithi kampuni ya Samsung, akiwa chini ya ulinzi baada ya kuhukumiwa
Spread the love

MRITHI aliyetarajia kurithi kampuni ya Samsung, Lee Jae-yong amehukumiwa kifungo cha miaka mitano na mahakama ya nchini Korea Kusini kwa kosa la rushwa, anaandika Jovina Patrick.

Lee ambaye pia anafahamika kama Jay Y Lee na kiongozi wa kampuni hiyo kubwa zaidi ya kutengeneza simu duniani, amekuwa kizuizini tangu mwezi februari akikabiliwa na tuhuma kadhaa za rushwa.

Miongoni mwa makosa aliyokabiliwa nayo ni utoaji rushwa, wizi wa mali ya umma na kuficha mali nje ya nchi.

Wakili wa Lee amesema watakata rufaa kupinga uamuzi uliotolewa na mahakama hiyo,”Tuna imani kwamba hukumu hii itabatilishwa,” wakili Song Wu-cheol amewaambia wanahabari baada ya kusomwa kwa hukumu hiyo.

Hata hivyo, uamuzi huo wa mahakama ni pigo kubwa kwa kampuni hiyo kubwa zaidi na inayofahamika zaidi duniani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!