Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili
Habari za Siasa

Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili

Spread the love

ESTHER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anaendelea na matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kufikishwa hospitalini hapo jana, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, John Stephen, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili amesema, Bulaya anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.

“Esther Bulaya aliletwa hapa kwetu jana usiku saa tano, na alitokea hospitali ya wilaya ya Tarime, yuko hapa na anaendelea vizuri na matibabu lakini hatuwezi kuweka wazi nini kinamsumbua, ” alisema

Bulaya alikimbizwa hospitalini jana baada ya kuzidiwa na kupoteza fahamu akiwa rumande alikokuwa ameshikiliwa na jeshi la polisi Kanda Maalum ya Tarime akituhumiwa kuhutubia mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!