Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali ya JPM yapigwa ‘dongo’
Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya JPM yapigwa ‘dongo’

Rais John Magufuli, Rais wa Tanzania. Picha ndogo Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye
Spread the love

WAZIRI Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ametoa tuhuma nzito kwa serikali ya awamu ya tano huku akisema kuwa haizingatii misingi ya sheria pamoja na kuheshimu utawala bora, anaandika Hellen Sisya.

Amesema serikali ya awamu ya tano imeshindwa kuheshimu mhimili wa Mahakama pamoja na Bunge na kwamba Mahakama Kuu ilitoa zuio la muda katika kumpora mashamba yake lakini, amri hiyo imepuuzwa.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika mapema leo hii katika ofisi za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kanda ya Pwani, zilizopo eneo la Magomeni jijini Dar es salaam, Sumaye amesema serikali imempokonya mashamba yake pasipo kujali zuio ambalo Mahakama Kuu.

“Kama nilivyokwisha eleza, tulifungua kesi mbili Mahakama Kuu kwa kufuata taratibu zote za kisheria, moja dhidi ya wavamizi na nyingine dhidi ya serikali”, amesema Sumaye

Mwanasiasa huyo amefafanua kuwa kesi ziko mahakamani na zinaendelea hata sasa na mahakama imeweka zuio la muda kwa shughuli yoyote kutoendelea katika eneo hilo na wahusika wote yaani wavamizi na serikali wana taarifa hiyo.

Sumaye ameweka wazi kwamba shamba hilo limetwaliwa na rais kwa maagizo ya kuligawa kwa wananchi huku ikidaiwa kwamba wavamizi wapewe kipaumbele.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!