Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili
Habari za Siasa

Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili

Spread the love

ESTHER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anaendelea na matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kufikishwa hospitalini hapo jana, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, John Stephen, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili amesema, Bulaya anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.

“Esther Bulaya aliletwa hapa kwetu jana usiku saa tano, na alitokea hospitali ya wilaya ya Tarime, yuko hapa na anaendelea vizuri na matibabu lakini hatuwezi kuweka wazi nini kinamsumbua, ” alisema

Bulaya alikimbizwa hospitalini jana baada ya kuzidiwa na kupoteza fahamu akiwa rumande alikokuwa ameshikiliwa na jeshi la polisi Kanda Maalum ya Tarime akituhumiwa kuhutubia mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!