Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaffo ‘ayananga’ maonesho ya nanenane
Habari Mchanganyiko

Jaffo ‘ayananga’ maonesho ya nanenane

Suleiman Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), Selemani Jafo amewashukia, Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa mikoa ya Dodoma na Singida kwa kushindwa kufanya maandalizi ya uhakika ya Nane nane kanda ya kati, anaandika Dany Tibason.

Jafo amesema kuwa inasikitisha kuona maonesho ya nanenane yanageuzwa kuwa soko la kuuza nguo za ndani na mabeseni ya kuogea watoto badala ya kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji.

Jaffo amesema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wakulima nanenane kanda ya kati yaliyofanyika katika kiwanja cha Nzuguni mjini hapa.

Akifunga madhimisho hayo amesema lengo la kuwepo kwa nane nane ni kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji ili kuwawezesha kutoa elimu bora kwa wakulima kulima kilimo chenye tija badala ya kile cha kijikimu.

Amesema haiwezekani maonesho ya nane nane ambayo yapo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji yakageuzwa kuwa sehemu ya kuuza beseni za kuogeshea watoto pamoja na kuuza nguo za ndani na mitumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!