WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama amesema wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini watakaoshindwa kutenga asilimia tano ya mapato kwa ajili ya vijana na wanawake watachukuliwa hatua, anaandika Dany Tibason.
Mbali na kutakiwa kutenga asilimia hizo pia Wakurugenzi wote wametakiwa kutenga maeneo ya kufanyia biashara ambazo zinafikaka kwa urahisi.
Mhagama amesema kumekuwa na tabia ya Wakurugenzi wengi kutenga maeneo ili mradi tu kutimiza wajibu, lakini maeneo hayo hayana miundombinu na wala hakuna wateja.
Leave a comment