Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaffo ‘ayananga’ maonesho ya nanenane
Habari Mchanganyiko

Jaffo ‘ayananga’ maonesho ya nanenane

Suleiman Jaffo, Naibu Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), Selemani Jafo amewashukia, Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa mikoa ya Dodoma na Singida kwa kushindwa kufanya maandalizi ya uhakika ya Nane nane kanda ya kati, anaandika Dany Tibason.

Jafo amesema kuwa inasikitisha kuona maonesho ya nanenane yanageuzwa kuwa soko la kuuza nguo za ndani na mabeseni ya kuogea watoto badala ya kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji.

Jaffo amesema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wakulima nanenane kanda ya kati yaliyofanyika katika kiwanja cha Nzuguni mjini hapa.

Akifunga madhimisho hayo amesema lengo la kuwepo kwa nane nane ni kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji ili kuwawezesha kutoa elimu bora kwa wakulima kulima kilimo chenye tija badala ya kile cha kijikimu.

Amesema haiwezekani maonesho ya nane nane ambayo yapo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji yakageuzwa kuwa sehemu ya kuuza beseni za kuogeshea watoto pamoja na kuuza nguo za ndani na mitumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!