Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga
Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga

Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amewatoa hofu wananchi wa Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga kwamba hakuna mtu atakayechukuliwa ardhi yake bila kulipwa, anaandika Mwandishi Wetu

Amesema serikali haitamuonea mwananchi yeyote kwa wale ambao maeneo yao yatapitiwa na miradi mbalimbali ya uboreshaji wa miundombinu ya kiuchumi.

Waziri amesema kila mmoja atalipwa fidia kwa mujibu wa sheria ili kuipisha miradi hiyo ambayo itaisadia Tanzania kufikia kwenye uchumi wa kati mwaka (2025).

Mbarawa aliyazungumza hayo mjini Shinyanga kwenye ziara yake fupi ya ukaguzi wa miradi mbalimbali inasimamiwa na wizara anayoingoza.

Amesemma serikali imedhamiria kujenga na kufufua miundombinu yake yote ya kiuchumi, ukiwamo huo uwanja wa ndege na bandari ya Isaka wilayani Kahama, miradi ambayo itasaidia kukuza sekta ya uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!