Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ACACIA yakubali kuilipa serikali
Habari Mchanganyiko

ACACIA yakubali kuilipa serikali

Spread the love

ACACIA Mining Limited imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia sita (6%) baada ya sheria ya madini kubadilishwa, anaandika Victoria Chance.

Kampuni hiyo inayomiliki makampuni ya uchimbaji wa madini ya ACACIA nchini imekubali kulipa mirabaha hiyo iliyowekwa katika sheria mpya ya madini.

Sheria hiyo mpya imeitaka kampuni hiyo kulipa asilimia sita ya mirabaha ikiwa ni ongezeko la asilimia mbili (2%) moja ikiwa ya usafirishaji kwenda nje.

ACACIA inaendelea kufuatilia matokeo hayo ya sheria mpya katika mwanga wa maendeleo yake mapya ya madini.

Ikumbukwe kuwa sheria hiyo ya madini ilikuwa mswada mnamo mwaka 2010 na imeanza kutekelezwa mwaka huu.

Aidha, ACACIA ilidaiwa kukwepa kodi hapo awali baada ya kamati ya wakaguzi wa serikali kuwasilisha ripoti ya masuala ya madini kwa Rais.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!