Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Umbali wa zahanati waongeza vifo vya wajawazito
Habari Mchanganyiko

Umbali wa zahanati waongeza vifo vya wajawazito

Mama mjamzito
Spread the love

ONGEZEKO la vifo vya wajawazito hapa nchini linachangiwa na umbali wa vituo vya afya katika halmashauri zilizopo vijijini pamoja na ubovu wa miundombinu, anaandika Esther Macha.

Stephen Africa, Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la HIMSO amesema kuwa wanawake wajawazito wanaoishi vijijini wataendelea kuwa katika hatari ya kupoteza maisha iwapo hawatasogezewa huduma za kiafya pamoja na kuboreshwa kwa miundombinu.

Alikuwa akizungumza katika mkutano mkuu wa shirika hilo mkoani Mbeya.

“Tafiti zilizofanywa na shirika la PATH mwaka 2012 lilibaini asimilia 61 ya wanawake nchini hawakuweza kujifungua kwenye vituo vya afya kutokana na umbali mrefu, asilimia 44 walikosa usafiri wa kuwafikisha kwenye vituo vya afya.

“Tafiti zingine zilifanywa mwaka 2010 juu ya ubora wa mfumo wa rufaa wa afya ya uzazi vijijini Tanzania ulionyesha kuwa mfumo huo ni muhimu katika kusaidia huduma za afya ya uzazi,” amesema.

Hata hivyo, ameeleza kuwa wanawake wengi hawazingatii ushauri  wa rufaa kutokana na changamoto ya ufinyu wa rasilimali fedha na miundombinu duni ya usafiri iliyopo vijijini.

Shirika la HIMSO linatoa huduma za kiafya katika halmashauri za Kyela, Rungwe na Busokelo zilizopo mkoani Mbeya, na kwa upande wa mkoa wa Songwe shirika hilo linatoa huduma zake katika wilaya ya Mbozi.

Kwa upande wake William Ntinika, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya amepongeza jitihada kubwa ambazo zinafanywa na shirika hilo katika kushughulikia afya ya uzazi kwa wanawake.

“Serikali inatambua na kuunga mkono jitihada za shirika hili katika  kusaidia makundi  ya wenye vipato duni na makundi maalum kama waishio na virusi vya Ukimwi, wajawazito, na watoto waishio  kwenye mazingira hatarishi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

Habari Mchanganyiko

Makonda autaka mgodi kubadilisha maisha ya wana-Geita

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa...

error: Content is protected !!