Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mgogoro Poli Tengefu la Loliondo wadumu miaka 25
Habari za Siasa

Mgogoro Poli Tengefu la Loliondo wadumu miaka 25

Makundi ya Ng'ombe yaliyokutwa katika Poro Tengefu la Loliondo
Spread the love

MBUNGE wa Viti Maalum, Catherine Magige (CCM) amehoji kuhusina na ni lini serikali itatatua mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo uliodumu zaidi ya miaka 25, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali leo bungeni, Catherine alidai kuwa katika Pori Tengefu wa Loliondo kumekuwa na mgogoro mkubwa hivyo ni lini serikali itatatua mgogoro huo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani amesema Desemba 2016, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alifanya ziara katika Wilaya ya Ngorongoro ambapo pamoja na mambo mengine alitoa maelekezo ya jinsi ya kupata ufumbuzi wa mgogoro huo.

Amesema katika utelekezaji wa agizo hilo kamati maalum shirikishi inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambapo iliundwa ili kupata mapendekezo ya namna ya kutatua migogoro hiyo.

‘’Kamati maalum ilifanya kazi yake kwa njia mbalimbali zikiwemo kufanya vikao na wadau mbalimbali kutembelea eneo lenyewe ili kujua hali halisi na kuandaa taarifa yenye mapendekezo ya namna kutatua mgogoro huo,’’ amesema

Naibu Waziri huyo amesema mapendekezo ya kamati hiyo yamewasilishwa kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

error: Content is protected !!