Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wazee wa mahakama kuongezewa posho
Habari Mchanganyiko

Wazee wa mahakama kuongezewa posho

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

SERIKALI inaangalia uwezekano wa kuongeza posho ya wazee wa mabaraza ya Mahakama kutokana na kiwango cha Sh. 5,000 kinacholipwa hivi sasa kwa wazee hao kuwa kidogo lakini pia kupunguza vitendo vya rushwa, anaandika Dany Tibason.

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Paramagamba Kabudi alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mbagala, Ali Mangungu (CCM).

Katika swali lake Mangungu alitaka kujua kama setikali haioni kuwa inachochea vitendo vya rushwa kwa kutoa kiasi hicho  kidogo cha posho kwa wazee hao .

Awali katika swali la msingi mbunge huyo alitaka kujua kama serikali haioni ni wakati muafaka sasa kwa serikali kuwaongezea posho wazee hususan katika Mahakama Kuu ya Dar es Salaam ambao wamekuwa wakisikika kesi nyingi zikiwemo za mauaji.

Akijibu swali hilo Kabudi amesema serikali itawaongezea posho wazee wa mahakama kwa kadri bajeti itakavyokuwa inapatikana.

Aidha amesema serikali inatambua mchango mkubwa wa wazee wa baraza katika mahakama nchini na umuhimu wa kutoa posho kama motisha na kwamba kutokana na umuhimu huo serikali ingetamani posho za wazee hao ziongezeke ili kuendana na hali ya uchumi.

Amesema kwa bahati mbaya posho hizo hutokana na bajeti ya matumizi mengineyo ambazo hutengwa na serikali kwa kila fungu.

Hata hivyo Prof. Kabudi amesema kwa mwaka wa fedha 2016/17, mahakama ya Tanzania ilitengewe kiasi cha Sh. 1.27 bilioni na mwaka 2017/18, mahakama imetenga Sh. 1.85 bilioni kwa ajili malipo ya posho ya wazee wa baraza. 

Amesema serikali itaendelea kutenga au kuongeza posho kwa malipo mbalimbali zikiwemo posho kwa ajili ya wazee wa baraza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Makonda autaka mgodi kubadilisha maisha ya wana-Geita

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ametoa wito kwa...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Je, miji ya Uingereza inafilisika?

Spread the loveMNAMO 1890, mwandishi mmoja wa habari Mmarekani aitwaye Julian Ralph...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

error: Content is protected !!