Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lisiwe ndumilakuwili – Kubenea
Habari za Siasa

Bunge lisiwe ndumilakuwili – Kubenea

Bunge likiendelea na vikao vyake
Spread the love

MBUNGE wa Ubungo, Saed Kubenea, amehoji uhalali wa Bunge kuwaadhibu wabunge wa upinzani na “kuwanyamazia” wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaandika Erasto Masalu.

Akizungumza bungeni leo asubuhi (Ijumaa), Kubenea amesema, kumejengeka utaratibu mbaya ndani ya Bunge hili wa kuwapendelea wabunge wa CCM na kuwanyonga wabunge wa upinzani.

Kubenea alitoa mfano wa Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Mayenga aliyedai kuwa wabunge wanaozungunzia vitendo vya utekaji na utesaji bungeni, wanatoa kauli hizo kwa kuwa wamehongwa.

Amesema, “…naibu Spika, wakati Mheahimiwa Lucy Mayenga anazungumza bungeni alidai kuwa wabunge wanaozungumzia utekaji wamehongwa. Nilipomtaka athibitishe au afute kauli yake, mwenyekiti alidai hakusikia.

“Akaahidi kusoma Hansard (kumbukumbu za Bunge), lakini mpaka leo hajatoa majibu. Lakini hata pale lipoendelea kuchangia, bado alisistiza kuwa ana ushahidi wa anachokisema.”

Amesema, kinyume na inavyokuwa kwa wabunge wa upinzani, kwamba hata pale ambapo wanafanya makosa madogo, huchukuliwa hatua, lakini wabunge wa CCM wanalindwa.
Kubenea alilitaka Bunge kutokuwa “ndumilakuwili” bali lisimame kwenye haki.

Akijibu muongozo huo, Naibu Spika, Tulia Ackson alimtaka Kubenea kufuatilia suala hilo kwenye utawala kwa kuwa ndani ya kanuni za Bunge, hakuna ukomo wa siku ya kutolewa hukumu.

Naye Kubenea akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu kutoka Dodoma, aliahidi kufuatilia suala hilo hadi kuhakikisha haki inatendeka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!