Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF wamtaka Sirro kuchukua hatua ‘mazombi’ ya Prof. Lipumba
Habari za SiasaTangulizi

CUF wamtaka Sirro kuchukua hatua ‘mazombi’ ya Prof. Lipumba

Julius Mtatiro, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF
Spread the love

KAMATI ya Uongozi ya Chama cha Wananchi ‘CUF’ imemtaka Kamishna wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro kuchukua hatua dhidi ya waliotekeleza uvamizi wa mkutano wa chama hicho mwishoni mwa wiki iliyopita, anaandika Hamisi Mguta.

Mkutano huo uliofanyika juzi na Mwenyekiti wa wilaya ya Kinondoni akiwa na waandishi wa habari kuzungumzia masuala mbalimbali ya chama hiko katika hoteli ya Vina iliyoko Mabibo uliingiliwa na watu waliovalia soksi usoni wakiwa na silaha za moto na marungu.

Akizungumza na waandishi wa Habari akiambatana na wajumbe wa kamati hiyo muda mfupi baada ya kukutana na Kamishna Sirro, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Julius Mtatiro amesema uamuzi huo ni baada ya kuona Jeshi la Polisi limekuwa kimya baada ya tukio la uvamizi huo kutokea.

“Tunaona hali inakoelekea ni mbaya na sisi wenye wanachama wengi tunashindwa kuwadhibiti watu wetu ikiwa polisi hawatawashughulikia wanaofanya matukio haya,” amesema Mtatiro.

Ameeleza kuwa ni mara ya 13 kutokea kwa matukio hayo na wamemuonya na kumomba asimamie polisi kufanya kazi yao katika tukio lililotokea Mabibo pamoja na matukio mengine yaliyopita.

“Hatutaki kuona nchi yetu inageuzwa kuwa sehemu ya umwagaji wa damu, hatutaki matukio ya watu kuuwawa yaanze kulipotiwa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!