Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CUF wamtaka Sirro kuchukua hatua ‘mazombi’ ya Prof. Lipumba
Habari za SiasaTangulizi

CUF wamtaka Sirro kuchukua hatua ‘mazombi’ ya Prof. Lipumba

Julius Mtatiro, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF
Spread the love

KAMATI ya Uongozi ya Chama cha Wananchi ‘CUF’ imemtaka Kamishna wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro kuchukua hatua dhidi ya waliotekeleza uvamizi wa mkutano wa chama hicho mwishoni mwa wiki iliyopita, anaandika Hamisi Mguta.

Mkutano huo uliofanyika juzi na Mwenyekiti wa wilaya ya Kinondoni akiwa na waandishi wa habari kuzungumzia masuala mbalimbali ya chama hiko katika hoteli ya Vina iliyoko Mabibo uliingiliwa na watu waliovalia soksi usoni wakiwa na silaha za moto na marungu.

Akizungumza na waandishi wa Habari akiambatana na wajumbe wa kamati hiyo muda mfupi baada ya kukutana na Kamishna Sirro, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Julius Mtatiro amesema uamuzi huo ni baada ya kuona Jeshi la Polisi limekuwa kimya baada ya tukio la uvamizi huo kutokea.

“Tunaona hali inakoelekea ni mbaya na sisi wenye wanachama wengi tunashindwa kuwadhibiti watu wetu ikiwa polisi hawatawashughulikia wanaofanya matukio haya,” amesema Mtatiro.

Ameeleza kuwa ni mara ya 13 kutokea kwa matukio hayo na wamemuonya na kumomba asimamie polisi kufanya kazi yao katika tukio lililotokea Mabibo pamoja na matukio mengine yaliyopita.

“Hatutaki kuona nchi yetu inageuzwa kuwa sehemu ya umwagaji wa damu, hatutaki matukio ya watu kuuwawa yaanze kulipotiwa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!